HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138703",
"previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138701",
"results": [
{
"id": 1403431,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403431/?format=api",
"text_counter": 78,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Sen. Olekina on 28.3.2024)"
},
{
"id": 1403432,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403432/?format=api",
"text_counter": 79,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Resumption of debate interrupted on 28.3.2024)"
},
{
"id": 1403433,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403433/?format=api",
"text_counter": 80,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Kingi",
"speaker_title": "The Speaker",
"speaker": null,
"content": " Proceed, Sen. Mwaruma."
},
{
"id": 1403434,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403434/?format=api",
"text_counter": 81,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Mwaruma",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13223,
"legal_name": "Johnes Mwashushe Mwaruma",
"slug": "johnes-mwashushe-mwaruma"
},
"content": "Bw. Spika, asante kwa kunipa fursa hii ili nichangie huu Hoja hii iliyoletwa na Senata wa Narok, Ledama Olekina, kuhusu malipo ya wanakandarasi ambao wamefanya kazi kwa serikali zetu za kaunti. Ukiangalia Hoja hii, hali ilivyo katika kaunti zetu ni kwamba kuna wanakandarasi wengi wamefanya kazi lakini hawajalipwa. Hili limepelekea hawa wanakandarasi kufunga biashara zao, wengine kujiua na benki nyingi sasa kukataa kuwapa mikopo wakandarasi wanaofanya kazi na serikali za kaunti. Hii imepelekea umaskini mwingi kwa wanakandarasi. Nakubaliana moja kwa moja ya kwamba ni vyema sheria ifuatwe wakati tunalipa wakandarasi kwa sababu sheria inasema kwamba wakati tumeanza mwaka mpya wa pesa, zile pesa za pending bills ziwe za kwanza kulipwa katika pesa zote zitakayoenda kwa serikali za kaunti. Bw. Spika, ufisadi ndio unaleta ukosefu wa kutolipwa kwa wanakandarasi. Hii ni kwa sababu nchini Kenya kuna jambo ambalo linaitwa asilimia kumi ama watu kutaka hongo ili kupeana kandarasi. Watu wengi katika kaunti zetu huwa wamepata pesa tayari kwa zile kandarasi zimefanyika. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1403435,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403435/?format=api",
"text_counter": 82,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Mwaruma",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13223,
"legal_name": "Johnes Mwashushe Mwaruma",
"slug": "johnes-mwashushe-mwaruma"
},
"content": "Na wakati wamepata pesa za kaunti badala kulipa wanakandarasi, wanatumia zile pesa ili kupeana zabuni mpya ili wapate asilimia kumi. Hii imepelekea malimbikizi ya pesa ambazo zinatakikana kulipwa wanakandarasi. Pesa hizi ni zaidi ya bilioni mia moja na saba zinazodaiwa Kaunti ya Nairobi. Kiambu ni shilingi bilioni tano nukta saba, Mombasa ni shilingi bilioni tatu nukta tisa na Taita-Taveta ni shilingi bilioni moja nukta mbili. Jambo la kushangaza ni kwamba hata wakati gatuzi zetu zinasema kwamba zimeweka katika bajeti pesa za kulipa wanakandarasi, pending bills au muswada unaosubiri haupungui. Taita-Taveta, kwa mfano, mwaka uliopita wa 2022/2023, walilipa shilingi milioni mia tatu hamsini. Lakini badala ya muswada unaosubiri kupungua unaongezeka. Kwa hivyo, nakubaliana na mapendekezo yaliyoko katika Hoja hii ya kwamba Mdhibiti wa Bajeti aangalie kwa ukaribu bili zilizosalia zinazolipwa na pesa ambazo anapitisha. Iwapo kaunti haijalipa muswada unaosuburi au bili zilizosalia, wasipewe pesa katika ule mgao uanofuata. Kuna kitu tunaona katika kaunti zetu. Kwa kimombo inaitwa"
},
{
"id": 1403436,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403436/?format=api",
"text_counter": 83,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "voided payments."
},
{
"id": 1403437,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403437/?format=api",
"text_counter": 84,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Mwaruma",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13223,
"legal_name": "Johnes Mwashushe Mwaruma",
"slug": "johnes-mwashushe-mwaruma"
},
"content": "Mara nyingine Mdhibiti wa Bajeti anapitisha pesa zilipwe kwa wanakandarasi. Lakini, anapopitisha malipo, hayalipwi kulingana na vile yamepitishwa, bali yanaenda kufanya mambo tofauti. Nafikiri ni vizuri Mhasibu Mkuu aangalie kwa ukaribu ni kwa nini kuna kuwa na voided payments . Jana kulikuwa na Taarifa ya Seneta wa Kisii akiuliza ni kwa nini kuna kuwa na"
},
{
"id": 1403438,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403438/?format=api",
"text_counter": 85,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "voided payments"
},
{
"id": 1403439,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403439/?format=api",
"text_counter": 86,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Mwaruma",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13223,
"legal_name": "Johnes Mwashushe Mwaruma",
"slug": "johnes-mwashushe-mwaruma"
},
"content": "nyingi. Ni vizuri kuwe na maelezo kamili ni kwa nini Mdhibiti wa Bajeti anapitisha pesa zilipwe kwa malipo aina fulani lakini hayo malipo yanasimamishwa na malipo yanaenda kwa kazi tofauti. Hili pia limepelekea kuongezeka kwa bili zilizosalia. Hii inaoenyesha ya kwamba hakuna huduma zitatolewa katika kaunti zetu. Hivyo basi, hili ni swala la kulivalia njuga. Hili ni swala ambalo kama Seneti, tunatakikana tusimamishe kazi zote ili kuangazia njia tutakayo tumia kuhakikisha ya kwamba pesa zinazopatikana kwa kaunti zinatumika kulipa bili zilizosalia. Na kwamba, zile kaunti ambazo hazitalipa bili zilizosalia kulingana na Kanuni 50(2) (3) ya Public Finance Management Act Regulations, kuwe na adhabu ya kutosha. Jambo lingine ambalo linapelekea kulimbikiza kwa bili zilizosalia ni bajeti ya ziada. Wakati tunatengeneza bajeti katika mwaka wa pesa, kuna pesa zinazotengwa za miradi kadha wa kadha. Kutengeneza bajeti kunatumia uhusishaji wa wananchi. Wanajua ni miradi gani wanataka ifanyike. Lakini, inafikia mahali kuna kuwa na bajeti za ziada ambazo zinatoa miradi yao. Wananchi hawaelewi ni kwa nini miradi yao haijafanyika. Mara nyingine, Maseneta wanalaumiwa ya kwamba pesa zinaibwa na hawasemi jambo lolote. Kwa sababu mradi wa wadi fulani ulikuwa katika bajeti lakini mwaka umeisha na ule mradi haujafanyika. Maseneta wanaendele kulaumiwa ya kwamba pesa zinaibwa na hawapigi kelele. Kumbe kuna bajeti ya ziada imefanyika ambayo haijahusisha mwananchi. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1403440,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1403440/?format=api",
"text_counter": 87,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Mwaruma",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13223,
"legal_name": "Johnes Mwashushe Mwaruma",
"slug": "johnes-mwashushe-mwaruma"
},
"content": "Kwa hivyo, hii Hoja inasema ya kwamba wakati bajeti ya ziada inapo tengenezwa, ni vizuri kuwe na uhusishaji wa jamii na wananchi wajue sababu za kuondoa mradi katika bajeti. Bw. Spika, la mwisho, wakati wa bajeti ya ziada, kama haijahusisha mwananchi, basi Mdhibiti wa Bajeti asipitishe hiyo bajeti. Nimeona kama kwetu Taita Taveta, wakati wa kuandaa bajeti ya ziada ambayo nafikiri ni ya tatu huu mwaka, pesa za wadi zilikuwa shilingi milioni ishirini. Lakini, zimepunguwa kwa kiasi cha shilingi milioni nane na zikabakia shilingi milioni kumi na mbili. Wananchi hawajui kama kama shilingi milioni nane zimetolewa zikaenda kujenga Aggregation Centre ama industrial park ambayo wao wenyewe hawajahusishwa. Nafikiri inatakikana tuchambue maandalizi ya bajeti kama Seneti. Hii ndio kazi ya Seneti ya ndani zaidi ambayo inatakikana ipatie kaunti zetu na wananchi meno ya kuhakikisha kwamba zile pesa wanapata kama ushuru zinatumika vile zilivyo pangiwa. La sivyo, tutakuwa tunapata malimbikizi ya bili zilizosalia, miradi haifanyiki na hatuelewi ni kwa nini, kumbe imetolewa kwa sababu ya bajeti ya ziada ambayo wananchi hawahusishwi na maandalizi yake. Hayo malimbikizi ya bili zilizosalia yanatakikana pia yaharamishwe na watu wafungwe. Singependa kuongea zaidi ya hapo. Ninaunga mkono hii Hoja iliyoletwa na Sen. Olekina. Ningerai wenzangu wapitishe Hoja tuangalie utekelezaji wa hayo mapendekezo ambayo yatapelekea kusaidia wananchi wetu wanaofanya kandarasi na serikali za kaunti. Hii italeta maendeleo, huduma na miradi ifanyike vizuri. Nashukuru sana kwa hii nafasi."
}
]
}