HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138855",
"previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138853",
"results": [
{
"id": 1404951,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404951/?format=api",
"text_counter": 327,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Thank you, Senator."
},
{
"id": 1404952,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404952/?format=api",
"text_counter": 328,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1404953,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404953/?format=api",
"text_counter": 329,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": "Hon. Senators, for the convenience of the House, we will reorganise the Order Paper. We move to the Motion by Sen. Mwinyihaji, Order No.21. Next Order."
},
{
"id": 1404954,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404954/?format=api",
"text_counter": 330,
"type": "heading",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "HOJA"
},
{
"id": 1404955,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404955/?format=api",
"text_counter": 331,
"type": "heading",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "KUIDHINISHWA KWA RUZUKU YA MASHARTI KWA UJENZI WA UWANJA WA MANISPAA YA MOMBASA"
},
{
"id": 1404956,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404956/?format=api",
"text_counter": 332,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Faki",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13211,
"legal_name": "Mohamed Faki Mwinyihaji",
"slug": "mohamed-faki-mwinyihaji-2"
},
"content": "Bw. Spika, asante kwa kunipa fursa hii. Kabla sijaendelea na Hoja hii, ningependa kuwaomba radhi baadhi ya Maseneta ambao walitarajia kwamba tutaizungumzia Hoja hii kwa lugha ya Kingereza. Ijapokuwa awali nilileta Hoja kwa lugha ya Kiingereza, nimeona itakuwa bora tuizungumze kwa lugha ya Kiswahili ili watu wengi nchini waweze kufuata, hasa watu wa Kaunti ya Mombasa, waweze kuelewa yale tunayo zungumzia. Hoja ni kuidhinishwa kwa ruzuku ya masharti kwa ujenzi wa uwanja wa Munisipaa ya Mombasa. KUFAHAMU KWAMBA sehemu ya pili ya Ratiba ya nne ya Katiba ya Kenya, inazipa serikali za kaunti jukumu la kuanzisha, kuendeleza, kusimamia, na kudumisha vifaa vya michezo na kitamaduni ambavyo ni pamoja na viwanja vya michezo, vituo vya utamaduni, na miundombinu mingine inayohusiana; IKIKUMBUKWA kuwa ukanda mzima wa Pwani nchini hauna uwanja wa kisasa, uliojengwa kwa viwango vya kimataifa hivyo kuwanyima wananchi manufaa yanayotokana na viwanja na vifaa kama hivyo; WASIWASI kwamba ujenzi wa uwanja wa michezo ya Manisipaa ya Mombasa, umekumbwa na ucheleweshaji, na vikwazo tangu kuanzishwa kwa mradi huo mwaka wa 2019 kutokana na matatizo ya kifedha, ambayo yameathiri utekelezaji wa mradi huo, na kunyima jamii ya eneo hilo uwanja unaohitajika; KWA HIVYO SASA, Bunge la Seneti, linaazimia kwamba Hazina ya Kitaifa na Wizara ya Maswala ya Vijana, Uchumi Ubinufu na Michezo, itengee Serikali ya Kaunti ya Mombasa, ruzuku ya masharti ya shilingi bilioni 1.7 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi uwanja wa Manisipaa wa Mombasa. Bw. Spika wa Muda, nimesimama kwa masikitiko kwamba ukanda mzima wa Pwani kwa sasa hauna uwanja wa kimataifa ambao unaweza kuchezewa mchezo wa mpira wa kimataifa. Uwanja ambao ulikuwa unatumika kwa muda mrefu ulikuwa ni uwanja wa Manisipaa ya Mombasa ambao ulijengwa kwa ufadhili wa Work for Aga Khan, mnamo mwaka wa 1957. Uwanja huu, uliandaa mchezo wa kimataifa mwaka wa 1962 wakati mchezo wa kwanza wa Gossage, ulichezwa. Gossage Cup ilikuwa inachezwa baina ya mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania. Baadaye iliitwa Confederation of East and Central African Federation (CECAFA). Mnamo mwaka wa 1962, Mombasa ilikuwa na uwanja wenye kiwango cha kimataifa, kwa wakati ule ambapo iliweza kuandaa michuano ya kimataifa. Vile vile,"
},
{
"id": 1404957,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404957/?format=api",
"text_counter": 333,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Faki",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13211,
"legal_name": "Mohamed Faki Mwinyihaji",
"slug": "mohamed-faki-mwinyihaji-2"
},
"content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1404958,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404958/?format=api",
"text_counter": 334,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Faki",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13211,
"legal_name": "Mohamed Faki Mwinyihaji",
"slug": "mohamed-faki-mwinyihaji-2"
},
"content": "baada ya hapo, uwanja huu umeandaa michuano mingi ya kimataifa, hususan CECAFA ambapo timu za Kenya, Uganda, Tanzania, Malawi, Zambia, Zimbabwe, zimewahi kucheza katika uwanja ule Na vile, mwaka wa 1996, uwanja huu uliandaa mechi ya kimataifa ya youth, ambao walikuwa washindi wa kwenda Olympic kati ya Kenya na Nigeria. Wachezaji wenye tajriba kubwa kama vile JJ Okocha na Nuan Kokanu waliweza kucheza katika uwanja ule. Ilizua hisia na uzalendo mkubwa kwa watu wa Kenya na watu wa Mombasa. Vile vile, uwanja huu umewalea wachezaji wengi kutoka Pwani. Vile, wengine walihamia bara, kwa mfano, marehemu, Ali Kajo, Marehemu, Ahmed Breik, Mahmoud Abass, ambaye alikuwa ni Kenya One kwa muda mrefu, na mwisho alichezea timu ya AFC Leopard, ambayo juzi, ililambishwa lolo na Gor Mahia hapa katika mchuano wa ‘Mashemeji Derby.’ Kwa hivyo, ni kiwanja kilicho na historia ya kusaidia pakubwa kuinua viwango vya mpira wa soka kabumbu katika eneo la Mombasa na Pwani kwa jumla. Ilipofika wakati wa ugatuzi, uwanja huu ulikuwa unasimamiwa na Baraza la Munispaa ya Mombasa. Ugatuzi ulipoingia, ukachukuliwa na Kaunti ya Mombasa. Nia na madhumuni ya Kaunti ya Mombasa ilikuwa ni kujenga uwanja wa kimataifa ambao utasaidia kuinua talanta katika eneo lile na kuandaa michuano ya kimataifa, ili kuleta biashara na maendeleo katika eneo la Pwani. Mnamo mwaka wa 2018, Kaunti ya Mombasa ilitoa mpango wa kuujenga upya uwanja ule na kutenga pesa za kutekeleza hilo. Mnamo mwaka wa 2017/2018, Kaunti ya Mombasa ilifanya vizuri sana katika ukusanyaji wa kodi Mjini Mombasa. Kwa lugha ya Kiingereza, inaitwa Source Revenue (OSR). Walifanya vyema mpaka Commission on Revenue Allocation (CRA) wakatoa ruzuku ya bilioni moja kama kiinua mgongo kwa Kaunti ya Mombasa kwa kukusanya pesa kupita matarajio yake. Kwa hivyo, mipango ilikuwa imefanya uwanja ule ujengwe kwa njia ya kudhibiti bajeti na kwa muda unaofaaa. Bahati mbaya ni kwamba Serikali Kuu ilipitsha amri mzigo mingi, ibebwe na Standard Gauge Railway (SGR). Kwa hivyo, biashara Mombasa ikaanguka na mapato ya Kaunti ya Mombasa pia yakaanguka. Baadaye, kukaingia janga la Korona mwaka wa 2020 mpaka 2021. Athari za Korona zikaathiri pakubwa, mapato ya Kaunti ya Mombasa na ya Serikali. Hivyo basi, ikawa Serikali ya Kaunti ya Mombasa haikuweza kupata pesa hizo. Hivi tunapo zungumza, imekuwa vigumu kwa Kaunti ya Mombasa kujenga uwanja huu kwa mkupuo mmoja. Zile pesa wanazoweka kwa bajeti yake, kwa mfano, bajeti ya mwaka jana, ilikuwa ni shilingi milioni themanini. Pesa hizi haziwezi kutosheleza ujenzi wa uwanja huu. Uwanja wenyewe umejengwa wa kisasa na utakuwa na uwanja wa mipira ya miguu, kidimbwi cha kuogelea cha hadhi ya Olympic, jumba la sanaa, ama auditorium ambalo litasaidia pakubwa kuinua sanaa, na pia jumba la mikutano., Uwanja huu utakuwa na uwezo wa kubeba, mashabiki, 18,000-20,000. Kwa hivyo, uwanja huu utakuwa wakimataifa. Kaunti ya Mombasa, ina hoteli na sehemu za kupumzika zenye viwango vya kimataifa. Kwa mfano, hoteli ya Serena, Whitesands,"
},
{
"id": 1404959,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404959/?format=api",
"text_counter": 335,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Faki",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13211,
"legal_name": "Mohamed Faki Mwinyihaji",
"slug": "mohamed-faki-mwinyihaji-2"
},
"content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1404960,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404960/?format=api",
"text_counter": 336,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Faki",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13211,
"legal_name": "Mohamed Faki Mwinyihaji",
"slug": "mohamed-faki-mwinyihaji-2"
},
"content": "Neptune na nyingine nyingi ambazo zina uwezo wa kubeba wageni wote watakaokuja kwa Kaunti ya Mombasa na kuhakikisha wamehudumiwa. Mwaka huu, Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano ya mabunge ya East Africa. Mashindano haya yamepangwa kufanywa katika Kaunti ya Mombasa. Kwa hivyo, kiwanja hiki kitakuwa na umuhimu zaidi kikikamilishwa ili kitumike wakati wa mchezo hii ya Bunge za East Africa. Uwanja tayari umetengenezwa. Iliyobakia sasa ni kuleta vifaa uwajani. Kinachoweza kuchelewesha labda ni kutengeneza ule uwanja wenyewe utakaotumika kucheza kandanda. Kwa ujenzi wa mambo mengine, ni vitu vichache vya kuwekwa kwa pamoja. Ninamsihi contractor amalize uwanja huo ili uwekwe tayari kwa matumizi. Sehemu yote ya Pwani kama nilivyotangulia kusema, hatuna uwanja kama huu. Hivyo basi, uwanja huu hautasaidia Mombasa peke yake, lakini utasaidia Pwani nzima kwa jumla. Tumeona kwamba talanta zipo katika eneo la Pwani. Lakini, haziwezi kukua kwa sababu hatuna nafasi ya kuleta timu za kimataifa kuja pale kucheza. Hatuna nafasi ya kuwaalika wakufunzi na timu zingine kwa sababu hatuna viwanja vya kisawasawa ambavyo wakufunzi wale watasaidiana kuinua talanta katika maeneo yetu. Kutokana na ukosefu wa uwanja ule, hali ya kandanda imeshuka katika eneo la Pwani. Tumeona vijana wengi wameingilia mihadarati na itikadi kali. Mwaka jana, Kamati ya Seneti ya Uhasibu ilienda kutathmini. Ilizuru uwanja ule na kuona kwamba unahitaji kukamilishwa. Juzi Serikali Kuu ilimtuma Waziri wa Michezo, Sanaa na Masuala ya Vijana. Alipozuru uwanja huo, aliahidi kwamba atasaidia kuujenga. Kuna Hazina ya Michezo, yaani Sports Fund, ambayo inatumika hususan kusaidia kujenga miundombinu na kununua vifaa vya michezo katika nchi yetu. Tunaomba pesa kwa sababu tunajua kuwa Serikali ni jungu kuu na ina fedha ambazo inaweza kutusaidia kumaliza ujenzi wa uwanja huo kwa haraka ili uweze kutumika na wananchi waweze kufurahia. Kenya imepata fursa ya kuandaa michuano ya kombe la mabingwa barani Afrika mwaka 2027. Mombasa na sehemu zingine za Pwani ziliteuliwa kuandaa michuano hiyo muhimu. Mwaka 2004, tulikuwa mbele katika ujenzi wa viwanja za michuano hiyo. Ni makosa kunyimwa fursa kama hii kwa sababu hatuna uwanja wa kimataifa ambao unaweza kutumika. Suala la viwanja sio tu la watu wa Pwani pekee, bali ni suala la kitaifa kwa sababu Mombasa ni sehemu ya Jamhuri ya Kenya. Kwa hivyo, hatufai kuachwa nyuma. Serikali ya Jubilee iliyoondoka mamlakani ilikuwa imeahidi kujenga stadia nane; moja katika kila mkoa. Hakuna hata moja iliyokamilika. Wakati huo, Mhe. Rais wa sasa, alikuwa Naibu wa Raisi. Alizungumza hadharani kwamba watajenga stadium moja kubwa katika kila mkoa. Hilo halikufanyika. Sisi watu wa Mombasa tunaomba atupe ruzuku ya masharti ya bilioni moja nukta saba ili tuweze kukamilisha mradi huo muhimu ambao utasaidia pakubwa nchi ya Kenya."
}
]
}