HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138858",
"previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=138856",
"results": [
{
"id": 1404981,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404981/?format=api",
"text_counter": 357,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "Thank you, Mr. Speaker, Sir. I support this Motion."
},
{
"id": 1404982,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404982/?format=api",
"text_counter": 358,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Senators",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "Kiswahili! Kiswahili!"
},
{
"id": 1404983,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404983/?format=api",
"text_counter": 359,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Order, Senators! He has the right to respond in either Kiswahili or English, whichever language he chooses is in order. Sen. Cherarkey, proceed."
},
{
"id": 1404984,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404984/?format=api",
"text_counter": 360,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "Bw. Spika wa Muda, sina uzoefu wa lugha ya Kiswahili lakini ninaunga mkono Hoja iliyoletwa na Seneta wa Mombasa, Sen. Faki. Viwanja vya michezo hapa nchini vipewe kipau mbele kwa ajili ya vijana. Ninaunga mkono sehemu moja ya Hoja alivyosema kuwa viwanja vitakavyotengenezwa katika sehemu mbalimbali za kaunti zetu zitasaidia vijana wapate mahali pa kufanya mazoezi ili wasitumie mihadarati na kufanya mambo ambayo siyo ya kistaarabu nchini. Kiongozi wa Walio Wachache katika Seneti ambaye ni hakimu mstaafu amesema kuwa Kaunti ya Nandi inajivunia kwa sababu ya kuwa na wanariadha waliobobea. Mwanariadha kama Kipchoge Keino na wale wengine wametoka Kaunti ya Nandi lakini hatuna viwanja vya michezo vya mazoezi. Ukiamka macheo utapata vijana wengine barabarani kule mashinani wakifanya mazoezi ya riadha. Jioni saa kumi na moja, ukiendesha gari ama kutembea kule mashambani utapata vijana wengine wanacheza voliboli. Hawana sehemu ama viwanja maalum ambavyo vimetengwa. Nashukuru Mhe. Rais William Ruto na Serikali yake kwa sababu mwaka jana, baada ya kuona kudhoofika na kuumia kwetu alitoa agizo kwa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo wajenge uwanja mpya mjini Kapsabet. Uwanja unaojengwa na serikali ya kaunti umejengwa zaidi ya miaka 14 kama vile jengo jipya la Bunge. Bajeti ya uwanja ule inaendelea kuongezeka. Ni aibu sana kuwa uwanja kwenye mji wa Kapsabet haujakamilika baada ya kutumia mabilioni ya pesa. Kwenye mji wa Nandi Hills, hakuna uwanja. Kukinyesha tu uwanja ulioko unaloa maji, vijana wanakosa nafasi ya kucheza. Uwanja huu unapaswa kujengwa na Serikali ya Kaunti ya Nandi lakini wamezembea. Kaunti ya Nandi imebarikiwa. Usiutazame mwili wangu huu, kwani nilikuwa mwanariadha shupavu. Karibu nishinde medali kwenye enzi zile zangu. Kaunti ya Nandi imebarikiwa na wanamichezo na wanariadha lakini hatuna uwanja uliotayari ili kuwapatia wanariadha na wanamichezo nafasi ya kufanya mazoezi. Gavana wa Kaunti ya Nandi alikuwa kwenye Kamati ya Seneti ya Uhasibu wa Fedha za Umma katika Kaunti."
},
{
"id": 1404985,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404985/?format=api",
"text_counter": 361,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1404986,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404986/?format=api",
"text_counter": 362,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "Bw. Spika wa Muda, ni aibu sana kwa sababu kama Kaunti ya Nandi, tunajivunia kuwa na wanariadha na hatuna uwanja wa kimataifa. Kama ujuavyo, wanariadha waliobobea, Bw. Eliud Kipchoge na Bw. Kipchoge Keino wanatoka katika Kaunti ya Nandi. Bw. Henry Rono ambaye tulimuzika majuzi na tunaendelea kuiombea familia, pia anatoka katika Kaunti ya Nandi. Pamela Jelimo na Janet Jepkosgei ambaye watu wengi wamempa jina la utani, Eldoret Express, pia wanatoka katika Kaunti ya Nandi. Hata hivyo, ni aibu kwa Kaunti ya Nandi na serikali za ugatuzi kwa sababu zimezembea. Wameshindwa hata kujenga kiwanja cha mbuzi ambako wanaweza fanya mazoezi. Mimi kama Seneta wa Kaunti ya Nandi naona aibu kwamba tunaipigania hapa. Nimekumbushwa kwamba kamati yetu ya masuala ya fedha inaangalia bajeti na tunaendelea kupigania pesa."
},
{
"id": 1404987,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404987/?format=api",
"text_counter": 363,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "Bw. Spika wa Muda, niko na sheria ambayo najaribu kuongeza asilimia ambayo inaenda katika kaunti, kutoka asilimia 15 mpaka 40. Ni aibu sana kuwa bilioni za pesa zimeenda katika Kaunti ya Nandi. Hata hivyo, Gavana wangu alipata muhula wa pili. Akiwa kule mashinani, alisema kwamba yeye hakushinda lakini alitumia mpira wa mkono ili apate muhula wa pili. Hiyo ndiyo sababu hatujaweza kuona maendeleo yeyote, hasa katika Kaunti ya Nandi. Nimeona Maseneta kama vile Sen. Abass na viongozi wa Walio Wengi na Walio Wachache Bungeni wakitaja Nandi. Kiongozi wa Walio Wachache amesema Nandi imejaa wanariadha. Lakini, hatuna viwanja vya michezo ambazo zinaweza tumika kuhakisha wanariadha wanafanya mazoezi ya kutosha. Ukienda katika Kaunti ya Uasin Gishu, utaona kiwanja cha 64 ambacho hakijakamilika. Ukienda katika Kaunti ya Elgeyo Markwet kuna uwanja wa mchezo unaoitwa Kamariny na kule Bomet kuna Bomet Green Stadium. Ninataka kumshukuru Mhe. Rais William Ruto na Serikali yake kwa sababu wakati tulisema Kericho Green Stadium ibadilishwe, imebadilishwa na kupewa jina la Kiburuku Chuma Wilson, ambaye alikuwa mwanariadha aliyebobea katika enzi zake. Ukienda katika Kaunti jirani ya Vihiga, Kisumu na sehemu za magharibi, tuko na wanariadha na wachezaji wa kandanda wengi walioheshimika. Kwa mfano, mchezaji maarufu Kadenge. Ndugu yangu Sen. (Dr.) Khalwale anatoka katika eneo la magharibu. Ni afadhali Kakamega wako na uwanja ambao wanaweza kutumia kufanya mazoezi. Hata hivyo, ulitengenezwa na Gavana aliyetoka. Kama Bunge la Seneti ni lazima tuchukuwe msimamo kidete na kuhakikisha kaunti zetu zimeweze kujua kwamba masuala ya michezo yamegatuliwa. Wachukuwe hatua kabambe na wahakikishe kwamba zile pesa ambazo wanaweka zinatumika kukuza talanta pale mashinani. Talanta Hela ilikuja na tunataka tujue inatumika vipi ili kuhakikisha vile viwanja ambavyo vinatakikana kujengwa katika taifa letu la Kenya vimejengwa. Tunapojitayarisha kwa dimba linalo kuja, najua Kaunti ya Mombasa, kaunti za kule magharibi kama vile Kakamega, Eldoret na nchi ya Uganda na Tanzania wanaweza"
},
{
"id": 1404988,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404988/?format=api",
"text_counter": 364,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1404989,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404989/?format=api",
"text_counter": 365,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Cherarkey",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13217,
"legal_name": "Cherarkey K Samson",
"slug": "cherarkey-k-samson"
},
"content": "kupewa nafasi ya kushiriki katika hilo dimba la mpira ambalo. Ni lazima tuwe tayari ikiwa dimba hilo litafulu. Bw. Spika wa Muda, mara nyingi Naibu wa Rais, Mhe. Rigathi Gachagua anapambana na mambo ya madawa ya kulevya na miharadati katika taifa letu la Kenya. Tukitaka kuangamiza janga hilo ni lazima tuhakikishe viwanja na kumbi za michezo zimetengenezwa ili vijana wapate mahali pakupata uraibu wa michezo mbalimbali katika taifa letu la Kenya. Nilikuwa na hoja tatu. Tunapoelekea katika michezo ya Olimpiki mwaka huu kule Paris, Ufaransa, nataka kuwaomba Wakenya tupeane ufadhili ambao tukonao ili kuhakikisha wanariadha ambao wanaelekea huko wamepata ufadhili wa kutosha ndio waweze kutuletea medali. Wakati wa wikendi, mwana riadha aliyebobea, Peris Chepchirchir, aliweza kuvunja rekodi mpya kule London. Hii ndio maana ninataka tuwape changamoto kwa kuwapa viwanja nafasi ya kutosha kufanya mazozi katika viwanja vyetu. Wakati tunaelekea muda wa michezo wa mwaka huu, wanariadha hawastahili kuwa na shida zozote. Tuliona yule murusha mkuki, Bw. Yego, alikuwa ameanza kuombaomba katika mitandao ya kijamii. Hiyo ni aibu sana ikizingatiwa tuko na kikapu maalumu ya mambo ya michezo katika taifa letu la Kenya. Nataka kumwambia Waziri wa Michezo kuwa tunamtegemea kuhakisha zile pesa za kusaidia hawa wanamichezo zinatumika vilivyo. Jambo lingine ni kuhakikisha tumefanya uchaguzi ya wale wanaosimamia riadha, voliboli na michezo mingine. Nimefurahi kuwa wakati kuliwa na mchezo wa ‘mashemeji’, ndugu yetu kinara wa Azimio alienda kuangalia mchezo huo ingawa hakuenda mazishini. Hata hivyo, tulikuwa tumeambiwa na ndugu yake kuwa alikuwa hajisikii vizuri. Nimefurahi kwa sababu walikusanya zaidi ya shilingi milioni nne nukta tano. Ikiwa tunataka tuweke viwanja vya mchezo, pesa zinazochukuliwa zinaweza kutosha. Bw. Spika wa Muda, naunga mkiono Hoja hii. Ninataka niwahakikishie wananchi wa Kenya na wanariadha kwa jumla, kuwa kama Bunge la Seneti tutafanya kazi pamoja. Nikimalizia kwa zile dakika chache ambazo zimebaki, nimemuona Seneta wa Narok. Jana nimeona katika mitandao kwamba kuna wale waakilishi wadi ambao wanapigwa katika mahafla pale mashinani wakati wanajaribu kuuliza maswali. Niliona mwakilishi wadi wa Mara ambaye anaitwa Kipng’eno Simba, akizabwa makofi. Hii si mara ya kwanza. Nilikuwa ninaona Gavana Tunai aliyetoka alikuwa na heshima kwa maswali. Gavana ole Ntutu ameanza kuwa mtukutu na hauwezi kumuuliza swali. Kwani Kaunti ya Narok iko Kenya ama inaendeshwa na wabeberu au wafedhuli? Lazima nimuulize Seneta wa Kaunti ya Narok alete Hoja hapa Seneti, kwa sababu hiyo ndiyo inaweza kuwa njia moja ya mtu kubanduliwa ofisini."
},
{
"id": 1404990,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1404990/?format=api",
"text_counter": 366,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Abdul Haji",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Sen. Cherarkey, nataka nikupe onyo kwamba umetoka nje ya mada ambayo tunaongelelea hapa. Ningependa ubaki katika Hoja ile tunaongelea. Wacha kutoka nje ya Hoja."
}
]
}