HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=139718",
"previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=139716",
"results": [
{
"id": 1413581,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413581/?format=api",
"text_counter": 637,
"type": "speech",
"speaker_name": "North Mugirango, UDA",
"speaker_title": "Hon. Joash Nyamoko",
"speaker": null,
"content": "The Departmental Committee on Lands engaged the sponsor of the Bill as highlighted and solicited comments from various stakeholders through an advertisement, which was done on 2nd October 2023. We received a number of memoranda from various stakeholders, including the National Land Commission, the Institution of Surveyors of Kenya, the Kenya Land Alliance, and the State Department of Lands and Physical Planning. I want to thank the Members of the Committee for their dedication and diligence in examining the Bill. I also thank the Office of the Speaker and the clerks who have served the Committee for their leadership and guidance throughout the legislative process. I also thank all those who were involved in the processing this Bill. I end by saying that these are very crucial exercises – the two amendments that are going to be done. They will give life to the National Land Commission. We have many cases that have been reported to the National Assembly. Some go to the Public Petitions Committee, and others to the National Land Commission. By effecting these amendments, I am very sure this will be a reprieve for the citizens of this country. Thank you, Hon. Temporary Speaker. With that, I second."
},
{
"id": 1413582,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413582/?format=api",
"text_counter": 638,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Martha Wangari",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": {
"id": 13123,
"legal_name": "Martha Wangari",
"slug": "martha-wangari"
},
"content": " Thank you."
},
{
"id": 1413583,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413583/?format=api",
"text_counter": 639,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Question proposed)"
},
{
"id": 1413584,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413584/?format=api",
"text_counter": 640,
"type": "speech",
"speaker_name": "Hon. Martha Wangari",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": {
"id": 13123,
"legal_name": "Martha Wangari",
"slug": "martha-wangari"
},
"content": "I will give this chance to Hon. Mishi. If not in the House, Hon. Zamzam."
},
{
"id": 1413585,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413585/?format=api",
"text_counter": 641,
"type": "speech",
"speaker_name": "Mombasa County, ODM",
"speaker_title": "Hon. Zamzam Mohammed",
"speaker": null,
"content": " Ahsante sana, Mhe. Spika wa Muda, kwa kunipa wakati huu nitoe mchango wangu kuhusu National Land Commission (NLC). Nampongeza ndugu yangu, Mhe. Owen Baya, kwa kuangalia historia hasa katika Ukanda wa Pwani. Hii Tume ya kuangalia mambo ya mashamba imekuwa ikisaidia sana kwa kutoa uwazi wa mambo yalivyo kule chini. Watu wetu wanateseka sana. Kwa mfano, baada ya Tume hii kuangazia dhuluma za kihistoria za mashamba, kuna watu mpaka sasa wanahangaishwa. Ni dhahiri shahiri kuwa Tume hii ilichaguliwa na kutengwa ili isaidie historia ya dhulma za mashamba na mambo kama hayo ili mnyonge aweze kupata haki yake. Sasa hivi tunavyozungumza, hata sisi pia tumeleta malalamishi ambayo yametoka katika kaunti zetu. Ukanda wa Pwani umekuwa ndio chanzo kikubwa cha kupata dhuluma za kihistoria za mashamba. Watu wetu wamekaa kama maskwota, na ukiangalia katika mashamba yale, kuna watu wamekaa zaidi ya miaka 200. Lakini, ile dhuluma wanafanyiwa, hasa ukiangalia wakazi wa pale Majengo, Mwembe Kuku, Bondeni na Kisiwani, bado wanalalamika na mpaka sasa hawajapata haki yao. Hii Tume ikiwekewa muda rasmi, itakuwa haina mwanya wa kujieleza zaidi. Hawa watu wamekaa zaidi ya miaka 200 kwenye shamba. Ukiangalia mpaka sasa, wanaambiwa watafurushwa kwenye mashamba yao. Mtu anajitokeza tu. Yeye amepotea na amekaa nje miaka yote. Lakini, anakuja kunadi na kuwapatia wale wazee wasiwasi, akiwaambia atawavunjia nyumba zao waondoke, wakati wamekuwa wakilipa kodi kwa zaidi ya miaka 50. Sheria iko wazi kuwa Wakenya wapewe ithibati ama hati miliki za mashamba ndio wakae kwa amani. Lakini, unapata kuna watu wanawanyanyasa, ndio maana Tume hii iliwekwa ili kuangalia maswala hayo. Naunga mjadala huu mkono ili Tume hii ikae na iwekwe wazi bila vizingiti vya miaka mitano, ndio tupate kutatua shida ambazo Wakenya wanapata. Napatia hii Tume ya Mashamba changamoto wafanye kesi nyingi, kwa sababu wamesikia mambo mengi ya mashamba na vilio vya watu wengi. Mpaka sasa, wamefanya kitu gani kuhakikisha kuwa watu wetu wanapata haki zao? Hii Tume ni nzuri sana, lakini naomba iweze kutatua matatizo yaliyoko ili Wakenya wapate haki zao. Kama tunavyoona wazee wetu, Council of Elders au Baraza la Wazee kule Mombasa wamelia sana. Mzee Sumba amelilia mashamba mpaka amezeeka, umri umekwenda, The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor"
},
{
"id": 1413586,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413586/?format=api",
"text_counter": 642,
"type": "speech",
"speaker_name": "Mombasa County, ODM",
"speaker_title": "Hon. Zamzam Mohammed",
"speaker": null,
"content": "lakini anatoa machozi kwa sababu wanavunjiwa manyumba katika mashamba wakati Serikali imenyamza. Namwambia ndugu yangu, Owen Baya, kwamba sote tumetoka Pwani, na tunajua matatizo ya watu wetu. Ndugu yangu uko katika mrengo wa Serikali, na naomba uingilie kati. Tunaitetea Tume ya Kitaifa ya Mashamba waweze kujibidiisha na kupigania haki za wanyonge, ili hao ndugu zetu waweze kupata title deeds na kukaa kwa amani. Wakati mwingine nikikaa huwa nalia machozi nikiona vile watu wangu wanavyodhalilishwa. Makaburi ya wazee mahali ambapo wamelala, wanahangaishwa. Mtu anatoka kule Oman na anakusanya rent ndani ya Mombasa ilhali, nchi yake ni nyingine. Naiomba Tume ya Kitaifa ya Mashamba waangazie Serikali na kuiambia hawa ni Wakenya wazaliwa, hata kama ni wanyonge na hawana pesa za kwenda mahakamani kujitetea. Lakini, Serikali itoke kuwatetea wanyonge, ambao ni Wakenya, wapate haki yao. Naunga mkono mjadala wa leo nikisema kuwa Tume ya Kitaifa ya Mashamba iwachwe ifanye kazi bila kuwekewa vizingiti vya wakati. Lakini, ijibidiishe kutoa matukio ambayo wamepata. Pia, watupatie udhabiti kuwa walisikiliza vilio vya watu fulani, wametatua na wakapata hati miliki za mashamba. Pengine mtu alipokonywa shamba lake, aweze kuregeshewa hilo shamba. Wasiwe wanakaa tu Nairobi na kuwaambia watu waje na wakija wanalala kwa mahoteli. Hatuwezi kukubali, kwa sababu hawana pesa, na kisha wanabaki hivyo hivyo. Wawajibike kama Tume ya Kitaifa ya Mashamba, kuhakikisha kuwa wanapatia watu wetu haki zao; na waonyeshe matokeo ya kazi waliyopewa, japokuwa wanalipwa na Mkenya yule wa chini. Naunga mkono nikisema Tume ya Kitaifa ya Mashamba isitolewe, isisitishwe, wala isiwekewe mipaka. Iwachwe huru. Miaka nenda miaka rudi, tuwe nayo, iwe inasaidia Wizara ya Ardhi kufanya kazi. Pale Ardhi House kuna uozo mkubwa sana. Leo tukisema tunawaachia wao ndio wachukue kila kitu wafanye, mtu ambaye amekaa ndani ya nyumba yake miaka 50 ama 100, ataskia mtu amekuja na hati miliki, akisema pale ni kwake. Uozo huu uko pale Ardhi"
},
{
"id": 1413587,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413587/?format=api",
"text_counter": 643,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "House"
},
{
"id": 1413588,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413588/?format=api",
"text_counter": 644,
"type": "speech",
"speaker_name": "Mombasa County, ODM",
"speaker_title": "Hon. Zamzam Mohammed",
"speaker": null,
"content": ". Ndio maana mimi, kama Mama Mombasa, nasema tusiwachie mamlaka yote Wizara ya Ardhi kwa sababu imetufeli miaka mingi sana. Tuwache mwanya wa kutatua mizozo ambayo iko, na kusikiliza walalahoi ambao wanalia kule chini, maanake mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kwa hivyo, mimi nalia pamoja na baba yangu, Hassan Sumba, nikisema watu wa Majengo, Mwembe Kuku na Bondeni wapewe haki zao. Ahsante sana Mhe. Spika."
},
{
"id": 1413589,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413589/?format=api",
"text_counter": 645,
"type": "heading",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "MOTION OF ADJOURNMENT ON A MATTER OF URGENT NATIONAL IMPORTANCE"
},
{
"id": 1413590,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1413590/?format=api",
"text_counter": 646,
"type": "heading",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "STATE OF SECURITY IN LAIKIPIA"
}
]
}