HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept
{
"count": 1608389,
"next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=148383",
"previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=148381",
"results": [
{
"id": 1502012,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502012/?format=api",
"text_counter": 214,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Madzayo",
"speaker_title": "The Senate Minority Leader",
"speaker": {
"id": 679,
"legal_name": "Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo",
"slug": "stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"
},
"content": "Pili ni kwamba, ilikuwa ni muhimu aweze kukemea ama aseme katika Hotuba yake kwamba, hakufurahia vitendo vilivyofanywa na polisi walipotumia nguvu zaidi kuliko walivyokuwa wamefunzwa kule Kiganjo, jinsi ya kupambana na kesi kama hiyo. Hawa walikuwa vijana wadogo, waliruka ukuta na kuenda dining room, wakakula chakula kilichokuwa pale. Wengine waliingia ndani ya Bunge na kusema waliyoyasema. Lakini kuna watoto wetu ambao waliumia. Bw. Spika wa Muda, sasa watu wamesonga mbele. Wale walioumia wakati wa mgomo, natumai kwamba Rais atatafakari na atachukua hatua ya kuona ya kwamba hao vijana wa Gen-Z watapata afueni katika hospitali; na kama kulikuwa na mazishi, pesa zao zilipwe na wale waliopata ajali, wapatiwe huduma. Pia ningependa tuzingatie kwamba elimu ndio msingi wa maendeleo. Mambo ya elimu yalikuwa muhimu sana katika Hotuba hii; hususan anafaa atueleze kwa nini hivi sasa katika historia ya Kenya tangu tupate Uhuru, kumekuwa na migomo nyingi katika kila sekta. Ya muhimu zaidi ni kwamba kumekuwa na migomo za walimu kuanzia university, Kenya National Union of Post Primary Education Teachers (KUPPET) na Kenya National Union of Teachers (KNUT). Jambo gani linazusha migomo hii? Hilo ni jambo muhimu ambalo angezingatia katika Hotuba yake ya mwaka huu. Angetueleza ni hatua gani Serikali inachukua kusuluhisha swala la migomo ya walimu ambayo inatendeka kila uchao. Hivi sasa tunapoongea maprofesa wa chuo cha Moi, University of Nairobi, na kwingine wamegoma. Ingekuwa muhimu zaidi kuona Rais akiweka swala hili katika Taarifa yake ambayo alihutubia Wakenya, mwaka huu. Lakini, hakuweka. Migomo hiyo inaendelea mpaka sasa na hajaweza kutupatia suluhu. Hili lilikuwa jukumu lake muhimu kuwaambia Wakenya ili watoto wetu ambao tunawapeleka university waweze kumaliza masomo yao wakati unaohitajika na sio kuketi kule na kumaliza course ya miaka minne kwa miaka sita. Hii haitakuwa jambo la heshima au jambo nzuri. Nataka kugusia swala la uchumi wa nchi yetu ya Kenya. Kwa sasa tunaona ya kwamba kuna afueni kidogo, lakini hii haijatosha. Afueni kidogo imeingia na tunaona bei ya vitu vidogo kama unga imerudi chini na pia mboga zinapatikana. Lakini mambo mengi ya kuweza kuchukua mkono, kuweka kwenye sahani na kuchukua chakula na kula, bado yako na shida. Mambo mengi bado ni magumu. Ingekuwa muhimu kama Rais angeweza kuangalia haya mambo. Bw. Spika wa Muda, tuko na mambo ya medical insurance covers; kuna SHA na SHIF. Rais angechukua nafasi ili kufafanua jambo hili. Hatuoni hizi insurance zote mbili zikifanya kazi kikamilifu. Wengi wamekwenda kupata matibabu katika mahospitali na wakaambiwa hawawezi kutibiwa kutumia hizo insurance. Mimi mwenyewa nilienda kumwona daktari wangu na nikamuuliza kwa nini sioni watu hapo wakitumia kadi zao za SHIF na SHA. Akasema hizo hawakubaliani nazo. Ilkiwa madaktari wenyewe wale professionals hawakubaliani na hizo, hii inamaanisha kwamba bado kuna shida. Rais anaweza kuwa na nia nzuri ya kuona ya kwamba kila mtu anapata huduma za kujifaidisha kiafya lakini ikifika wakati wa implementation wengi wanambwaga Rais. The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1502013,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502013/?format=api",
"text_counter": 215,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Madzayo",
"speaker_title": "The Senate Minority Leader",
"speaker": {
"id": 679,
"legal_name": "Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo",
"slug": "stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"
},
"content": "Inaweza kuwa sio makosa yake. Yeye anafikiria kwamba watu wana implement, lakini watu wengine wanamchelewesha katika tegemeo lake la kuwasaidia Wakenya. Hivi sasa, hizo medical covers za SHIF na SHA, zote ziko na shida ama hazifanyi kazi. Bw. Spika wa Muda, vile vile, mawaziri wake wanafaa kutimiza yale anayoyasema Rais. Lakini mara nyingi tunaona jambo la kusikitisha ambapo Rais anaelekeza kitu lakini jambo hili linakosa kutekelezwa. Wale basi, wanambwaga Rais. Kuna haja gani Rais aseme kwamba kutakuwa na Collective Bargaining Agreement (CBA) na inafaa kutiwa kidole na Waziri wa Elimu ama Waziri wa Afya; ambaye anafaa kutekeleza mishahara fulani baada ya miaka miwili alafu asitekeleze jukumu hilo? Hii ndio inaleta mambo ya migomo. Ingekuwa bora Rais awaambie watu wake kwamba: Kutoka wakati huu sitaki Waziri wangu atie sahihi CBA ya wafanyikazi bila kuona hali ya uchumi au kuona kwamba Serikali itatimiza wajibu wake wa kukamilisha deni la walimu au watekelezaji kazi katika pande zote zinazotakikana kama afya na zinginezo. Bw. Spika wa Muda, Rais katika Hotuba yake aliongea vizuri kuhusu---"
},
{
"id": 1502014,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502014/?format=api",
"text_counter": 216,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Wakili Sigei",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Kindly add the Senate Minority Leader three minutes to conclude."
},
{
"id": 1502015,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502015/?format=api",
"text_counter": 217,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Madzayo",
"speaker_title": "The Senate Minority Leader",
"speaker": {
"id": 679,
"legal_name": "Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo",
"slug": "stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"
},
"content": " Kindly add me five."
},
{
"id": 1502016,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502016/?format=api",
"text_counter": 218,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Wakili Sigei",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Three minutes. I will consider that request once the three are over. Proceed."
},
{
"id": 1502017,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502017/?format=api",
"text_counter": 219,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Madzayo",
"speaker_title": "The Senate Minority Leader",
"speaker": {
"id": 679,
"legal_name": "Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo",
"slug": "stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"
},
"content": " I want to touch on important aspects. Jambo la kwanza ni kuwa, Rais aligusia mambo mengi mazuri. Aliongea kuhusu sukari, mahindi, kahawa, na majani chai. Kimaendeleo, zitasaidia namna gani? Kati ya mimea aliyozungumzia, kuna mimea miwili muhimu sana kutoka sehemu ninayotoka. Upande wa Kilifi kunakuzwa korosho na mananasi. Mkorosho ni mmea muhimu sana kwa maisha ya wakulima kule, pamoja na mananasi. Vitu vingi vinaweza kupatikana kwa urahisi kwa sababu ile ardhi inakuza mmea kama mkorosho. Ingekuwa vyema kama Rais angezungumzia hatua ambazo Serikali imechukuwa kutenga pesa zitakazopewa wakulima hawa wanaopanda na kuuza korosho, mananasi na maembe, kwa sababu hawa pia ni wanabiashara kule. Hivi sasa tunajipata katika hali ya uchochole kule Kilifi. Kulikuwa na maendeleo sana lakini hivi sasa hakuna kazi, na vijana hawa wameketi tu. Watu hawa wanaishia kukula muguka na kutenda maovu. Ikiwa Rais anapanga chochote hivi sasa, anafaa kutabaini kuwa mkorosho ndani ya Kaunti ya Kilifi unaweza kuwasaidia watu wengi kwa kupata mapato ya kazi. Mwisho, nampa kongole Rais kuhusu mambo ya Adani. Huyu ni mtu ambaye pengine angezorotesha nchi yetu katika hali ya uchumi. Lakini aliona mbele na kuamua kuwa ni bora kuwaambia Wakenya kuwa hiyo njia haifai. Zaidi ni kuwa, tuliona President Trump mwenyewe akikataa hizo deal za Adani. Serikali ya Amerika pia ikasema kuwa ashikwe na hatimaye hakumaliza siku 24. Sio kama sisi ambao tukielekeza mtu fulani ashikwe anaweza kupotea kwa wiki nzima. Kule Amerika maagizo yalipita kuwa Adani ashikwe kabla ya masaa 24. Hatua ambayo Rais alichukuwa ilikuwa safi. Hii ni pamoja na hatua ya Kenya Electricity The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
},
{
"id": 1502018,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502018/?format=api",
"text_counter": 220,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Madzayo",
"speaker_title": "The Senate Minority Leader",
"speaker": {
"id": 679,
"legal_name": "Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo",
"slug": "stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"
},
"content": "Transmission Company (KETRACO) wasimamishe biashara yao pamoja na ile ya Adani kutengeneza airports zetu. Hili ni jambo ambalo litasaidia uchumi wa nchi hii kutoweza kupoteza pesa ambazo tunahijati zaidi kwa kuzikinga na ufisadi."
},
{
"id": 1502019,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502019/?format=api",
"text_counter": 221,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. Wakili Sigei",
"speaker_title": "The Temporary Speaker",
"speaker": null,
"content": " Senate Minority Leader, you note that you were unable to fully utilize the three minutes I added you. I appreciate the timekeeping, so that the rest of your colleagues who are interested in contributing can also get an opportunity. I now call upon Sen. (Dr.) Murango."
},
{
"id": 1502020,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502020/?format=api",
"text_counter": 222,
"type": "speech",
"speaker_name": "Sen. (Dr.) Murango",
"speaker_title": "",
"speaker": {
"id": 13585,
"legal_name": "Murango James Kamau",
"slug": "murango-james-kamau"
},
"content": "Asante sana, Bw. Spika wa Muda. Kwanza ningetaka ni muarifu Sen. Madzayo kwamba---"
},
{
"id": 1502021,
"url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502021/?format=api",
"text_counter": 223,
"type": "scene",
"speaker_name": "",
"speaker_title": "",
"speaker": null,
"content": "(Sen. Madzayo spoke off record)"
}
]
}