GET /api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=148430
HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept

{
    "count": 1608389,
    "next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=148431",
    "previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=148429",
    "results": [
        {
            "id": 1502492,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502492/?format=api",
            "text_counter": 98,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": {
                "id": 16,
                "legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
                "slug": "farah-maalim"
            },
            "content": "The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor."
        },
        {
            "id": 1502493,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502493/?format=api",
            "text_counter": 99,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Likoni, ODM",
            "speaker_title": "Hon. Mishi Mboko",
            "speaker": null,
            "content": " Ahsante, Mhe. Spika wa Muda. Natoa kongole kwa Hotuba ya Rais Daktari William Ruto. Katika Hotuba yake, alizungumzia mambo mengi sana. Jambo la kwanza, nakubaliana na yeye kwamba shilingi yetu imejizatiti na kufika KSh129 kwa US$ moja kutoka Ksh162. Hii inamaanisha kuwa tunaelekea katika mkondo sawia kiuchumi. Hivyo basi, jambo hili linaweza kuwashawishi sana wawekezaji kutoka mataifa tofauti na wale wanaotoka nchini pamoja na wafanyibiashara. Hivyo, tumeona shilingi yetu imenawiri na kujisatiti juu ya dola. Kwa upande wa Special Economic Zones kama za kule kwangu Likoni, mpaka sasa, takriban wawekezaji 94 wameweza kuleta barua za kusema watawekeza katika sehemu ile. Hii ina maana kuwa uchumi wa taifa la Kenya utaweza kupanuka na ajira zitakuwa nyingi kwa vijana wetu. Mhe Rais pia alizungumzia njia ya kutafuta ajira pasi na zile zilioko katika taifa letu. Tumeona ametafuta ajira katika bara Uropa, Asia na zinginezo. Hili ni jambo nzuri. Lakini kuna wahusika wanamuangusha Mhe. Rais. Nafasi hizo zinavyotokea, hazisambazwi kwa njia ya usawa na uadilifu kwa kaunti zetu 47. Haswa, tukiangalia kuna kaunti kama za kaskazini mashariki, sehemu za Pwani na zile zinginezo, nafasi hizo hazifiki. Hivyo basi, Wakenya wanaona pengine jambo hili halifanyiki, na kumbe linafanyika tena kwa hesabu za juu sana. Wakenya zaidi ya laki moja wameenda kufanya kazi katika nchi za nje. Kwa hivyo, tunasema wahusika waangaliwe waweke ukenya kwa jambo hili. Vile vile, kwa kufufua viwanda vyetu vya sukari, uchumi umeimarika. Pili, tunajenga ajira. Vile vile, tunapunguza gharama ya maisha kwa wakenya kwa sababu bei ya sukari itashuka. Shilingi inavyonawiri, tunaona bei ya bidhaa kama unga na mafuta imeshuka. Kwa hivyo, kuboresha viwanda vya sukari ni jambo nzuri sana. Hivyo basi, tunaomba kiwanda cha Ramisi kule Kwale katika eneo la Pwani kiweze kufufuliwa, kuimarishwa ili uchumi uweze kupanuka. Jambo lingine nataka kulizungumzia ni swala la elimu. Rais alilizungumzia sana swala la elimu. Alisema walimu wengi sana waliandikwa kazi wakati wa awali na hivi sasa pia, walimu takriban 20,000 wataweza kuandikwa kazi. Namwambia Mheshimiwa Rais kuwa tunampongeza kwa jambo hili. Lakini ninarudia kusema kuwa wahusika waweze kusambaza nafasi hizo za walimu katika kaunti zetu 47 ili waone kuna uadilifu na usawa. Kwa Kiingereza, tunasema equity na equality. Maanake, tukizungumzia uadalifu na usawa, ni zile sehemu ambazo zimekuwa na changamoto zipate walimu zaidi. Swala lingine ni lile la Adani. Nampongeza Rais kwa kukomesha sakata hiyo. Kwa sababu lazima uwekezaji ufuate utaratibu na sheria na utumie fedha yenye haitamuumiza mwananchi katika taifa ya Kenya. Jambo lingine ni dhuluma za kijinsia, haswa kwa watoto wetu wa kike. Tumeona watoto wetu wakitekwa nyara na kuuliwa kikatili. Kwa swala hili, vitengo vya usalama na ujasusi lazima vijizatiti ili tuweke usalama kwa akina mama zetu, wasichana na vijana. Jambo la mwisho, alizungumzia kuhusu umoja wa mataifa…"
        },
        {
            "id": 1502494,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502494/?format=api",
            "text_counter": 100,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": {
                "id": 16,
                "legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
                "slug": "farah-maalim"
            },
            "content": " Mpe nusu dakika."
        },
        {
            "id": 1502495,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502495/?format=api",
            "text_counter": 101,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Likoni, ODM",
            "speaker_title": "Hon. Mishi Mboko",
            "speaker": null,
            "content": " Alizungumzia umoja wa taifa. Nampongeza kwa kuweza kuleta uwiano wakati tulikuwa na ghasia zile za Gen-Z . Tunajua ya kwamba umoja wetu ni nguvu yetu. Kama hangeleta viongozi wengine ili tuwe na uwiano, leo tungekuwa wakimbizi katika taifa letu la Kenya. Tungeenda Uganda na Tanzania kutafuta makao. Kwa hivyo, ni vizuri tutambue ya kwamba sote ni Wakenya. Kama ulikuwa Upinzani, sasa sote ni Wakenya. Ni bora Wakenya wote wafaidike. Mambo ya kuwa na shares ..."
        },
        {
            "id": 1502496,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502496/?format=api",
            "text_counter": 102,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": {
                "id": 16,
                "legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
                "slug": "farah-maalim"
            },
            "content": " Mheshimiwa Ruweida Obo."
        },
        {
            "id": 1502497,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502497/?format=api",
            "text_counter": 103,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Lamu East, JP",
            "speaker_title": "Hon. Ruweida Mohamed",
            "speaker": {
                "id": 2100,
                "legal_name": "Shariff Athman Ali",
                "slug": "shariff-athman-ali"
            },
            "content": " Ahsante, Mhe. Naibu Spika wa Muda, kwa kunipa nafasi ya kuchangia mjadala kuhusu Hotuba ya Rais. Kusema kweli, Rais ni msikivu; yaani anasikiliza maneno. Hiyo ni sifa ya mwanadamu mzuri. Katika swala la Adani, kule"
        },
        {
            "id": 1502498,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502498/?format=api",
            "text_counter": 104,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Lamu East, JP",
            "speaker_title": "Hon. Ruweida Mohamed",
            "speaker": {
                "id": 2100,
                "legal_name": "Shariff Athman Ali",
                "slug": "shariff-athman-ali"
            },
            "content": "The electronic version of the Official Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Hansard Editor."
        },
        {
            "id": 1502499,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502499/?format=api",
            "text_counter": 105,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Lamu East, JP",
            "speaker_title": "Hon. Ruweida Mohamed",
            "speaker": {
                "id": 2100,
                "legal_name": "Shariff Athman Ali",
                "slug": "shariff-athman-ali"
            },
            "content": "kukataaa kwake kunatokana na kusikiliza. Hata hivyo, Mamlaka ya Kusimamia Viwanja vya Ndege Nchini (KAA) imepewa nafasi tena. Tunataka Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta uwe sawa na viwanja vingine vya ndege, kama vile Doha. Kuna Wakenya wengi kule. Ukiingia Doha, utafikiri uko katika Uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta. Watu wengi wametoka makwao kwa sababu ya shida za kiulimwengu. Ikiwa Airport itaendelezwa vizuri, walio nchini wataandikwa kazi na hata wale watakaotaka kurudi nchini wanaweza kurudi na kufanya kazi nzuri. Kwa hivyo, nataka kuambia KAA kuwa, kwa kuwa President amesitisha Adani, ni lazima wajitahidi Airport iwe nzuri. Mambo madogo madogo yamewashinda kufanya, kwa mfano, ukiingia airport zote Kenya, utakachoona ni jinsi ambavyo taxi zipo na vyoo vilivyo. Ukivitazama tu, utajua ni sura ya Kenya. Vitu vidogo vimewashinda. Ukiangalia vyoo ni vichache na usafi sio wa standard kama zile za viwanja vingine vya ndege. Upande wa taxi, abiria wanavutwavutwa ni kama wako katika Soko la Kongowea, Mombasa. Wenye taxi hawawezi kupanga laini. Niliuliza hili swali wakati mmoja na hata Waziri akaalikwa hapa, lakini hilo la laini halijawahi kufanyika. Sijui sababu ni nini. Mimi hamu yangu kubwa ni airport ibadilike iwe kama airports za mataifa mengine. Huwa tunaambiwa kuwa hapa East Africa, sisi ndio big brother. Lakini airport zetu zinatoa sura mbaya ya Kenya. Nilipendezwa na hutuba ya Rais na ninampongeza kwa mengi aliyosema. Rais kwa kweli anafaa kupewa muda. Ana nia nzuri ya kuiendeleza nchi hii. Akipewa muda, atatekeleza na mambo yatabadilika. Rais alizungumza kuhusu madeni ya kitaifa kuwa mengi alipoingia uongozini. Hata hivyo, hakuongeza madeni. Alitumia hekima. Angeongeza madeni, tungepigwa mnada kama nchi zingine. Inafaaa Wakenya waangalie jinsi ambavyo haya mambo yanavyoenda. Wasiwe tu wakiweka lawama. Sasa hivi, Rais ametuliza taifa na wakenya wamefurahi. Rais alizungumza juu ya kupunguza matumizi na ubadhirifu katika Speech yake. Hilo ni jambo nzuri ambalo Wakenya walitaka kulisikia. Kusema ukweli, Kenya inajiweza. Huwa inaporwa lakini bado husimama. Jee, ikiwa haitaporwa, si Kenya itakuwa mbali zaidi? Rais alizungumza juu ya bei ya bidhaa kupungua na ni ukweli bei zimepungua. Ukweli unafaa kusemwa. Kuna bidhaa kama unga ambazo zilikuwa ghali na kwa sasa bei yao imerudi chini. Kwa hilo, tunafaa kumpongeza Rais. Mtu akifanya mema, aambiwe amefanya mema. Kama wenzangu walivyo zungumza, shilingi ya Kenya imepata thamani dhidi ya dola. Ilivyokuwa awali ni tofauti na sasa. Wanaofanya biashara wameona utofauti huo. Hapo ninampongeza. Suala la kuwaandika waalimu kazi ni jambo nzuri. Maeneo bunge yetu hufanya mitihani sawa na maeneo bunge mengine. Hayafanyi mitihani tofauti. Shule ya upili ya Siyu ilikuwa ya mwisho kule Lamu East. Hata hivyo, tatizo halikuwa la shule. Wanafunzi hawajawahi kumwona mwalimu wa chemistry tangu shule hiyo ijengwe. Watatatuliwa vipi? Naomba waalimu waandikwe. Najua tuko kwa mpangilio katika Serikali hii. Kitakachopatikana tutakipata. Kwa afya, sisi kama Wabunge tutie bidii ili watu wetu wajiandikishe katika mpangilio wa bima ya afya. Ni mpangilio mzuri na utawasaidia sana Wakenya. Kuhusu nyumba, huo ni mpangilio mzuri. Nyumba zitasaidia na itakuwa legacy ya Rais…"
        },
        {
            "id": 1502500,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502500/?format=api",
            "text_counter": 106,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Hon. Farah Maalim",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": {
                "id": 16,
                "legal_name": "Farah Maalim Mohamed",
                "slug": "farah-maalim"
            },
            "content": " Mpe nusu ya dakika moja."
        },
        {
            "id": 1502501,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1502501/?format=api",
            "text_counter": 107,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Lamu East, JP",
            "speaker_title": "Hon. Ruweida Mohamed",
            "speaker": {
                "id": 2100,
                "legal_name": "Shariff Athman Ali",
                "slug": "shariff-athman-ali"
            },
            "content": " Hili jambo likifaulu, itakuwa legacy ya Rais. Rais alizungumza juu ya mambo ya ICT hubs . Hilo ni jambo muhimu sana kule Kiunga kwa sababu ipo mbali sana na Huduma Centre. Kiunga haipati services za Serikali. Itasaidia sana."
        }
    ]
}