GET /api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=155218
HTTP 200 OK
Allow: GET, POST, HEAD, OPTIONS
Content-Type: application/json
Vary: Accept

{
    "count": 1608389,
    "next": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=155219",
    "previous": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/?format=api&page=155217",
    "results": [
        {
            "id": 1570372,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570372/?format=api",
            "text_counter": 263,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Nakumbuka Seneti iliyopita tuliketi hapa zaidi ya vikao kumi bila makubaliano, lakini dakika ya mwisho tulikubaliana. Mpangilio wa ugavi uliotumiwa katika muhula wa tatu wa ugavi, ndiyo huo unaotumika wakati huu. Wakati ule watu walijadiliana na mambo mengi yalifanywa. Kuliundwa Kamati iliyokuwa ikiongozwa na Sen. Sakaja na Spika wa Bunge la Kitaifa wakati huu, Mhe. Wetangula. Tuliongea mengi na kukubaliana."
        },
        {
            "id": 1570373,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570373/?format=api",
            "text_counter": 264,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Ninasema hivi kwa sababu Sen. Mungatana alipokuwa akichangia alisema ya kwamba waliokuja nyuma wameleta kuchanganya yaliyokuwa yamezungumziwa hapo asubuhu. La hasha! Si kuchanganya; ni kuleta mwamko mpya, fikira na nguvu mpya. Watu wanapojadiliana, Wazungu husema ni mjinga tu asiyebadilisha mawazo. Wanaoleta mawazo mapya hata wao wanapaswa kusikilizwa."
        },
        {
            "id": 1570374,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570374/?format=api",
            "text_counter": 265,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
        },
        {
            "id": 1570375,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570375/?format=api",
            "text_counter": 266,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Bi. Spika wa Muda, kwanza kabisa ijulikane wazi kwamba pesa zinapaswa kufuata majukumu. Majukumu mengi yamepelekwa katika kaunti zetu lakini pesa zinabaki katika Serikali ya Kitaifa. Ikiwa hatutalivalia njuga jambo hili la pesa kufuata majukumu, tutakuwa tukipigania mkoba mdogo wa pesa, lakini mkubwa unao Serekali ya Kitaifa. Sisi tunapigana hapa lakini hatuwezi kufuatilia mahali palipo na hela kwa sababu majukumu mengi ambayo yamepelekwa katika kaunti zetu hayajafuatwa na pesa zake. Kwa Mfano, Mwenyekiki wa Kamati ya Afya yuko pamoja na sisi hapa. Hela nyingi za afya ziko katika Serekali ya Kitaifa ilhali Serikali imebaki na jukumu la sera na hospitali za kitaifa karibu tano ambazo ni Moi Teaching and Referral Hospital (MTRH), Kenya National Teaching and Referral Hospital, National Spinal Injury Referral Hospital, Kenyatta University Teaching and Referral Hospital na ile ya Mathari National Teaching and Referral Hospital. Hizo ndizo tu za Serikali ya Kitaifa ilhali asili mia 70 ya pesa zinabaki huko."
        },
        {
            "id": 1570376,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570376/?format=api",
            "text_counter": 267,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Mfano kuhusu barabara, Katiba inasema barabara zimegawanya mara mbili, za gatuzi na za kitaifa. Hata hivyo kuna halmashauri na taasisi kama vile Kenya Rural Roads Authority (KeRRA), Kenya Urban Roads Authrotity (KURA) na Kenya National Highways Authority (KeNHA) ilhali hizo pesa zingepelekwa moja kwa moja katika gatuzi zetu kwa sababu kuna aina mbili pekee. KeNHA ingebaki ikishughulikia barabara za kitaifa ilhali KeRRA na KURA zipelekwe katika gatuzi zetu kwa sababu huwa wanashughulikia barabara zilizo katika gatuzi zetu."
        },
        {
            "id": 1570377,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570377/?format=api",
            "text_counter": 268,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Tunapoongea kuhusu pesa ni vizuri tuwajibike vizuri na kusema kwamba gatuzi zinapaswa kuangaliwa. Kwa mfano hela zinazopewa kaunti ya Laikipia na majukumu tunayotakiwa kufanya pale, hizo hela ni chache sana. Hazitoshi. Kwa sababu leo asubuhi tulikuwa na huu mdahalo wa kujadili tutakavyoweza kuongeza hela zinakwenda katika kaunti ndogo kuliwekwa Kshs2 billioni kama hatua ya kuleta pesa za usawazishaji. Hizo fedha ni nzuri kwa sababu walionekana wana nia lakini hazitoshi. Pendekezo langu ni kuwa tuongeze ziwe shilingi bilioni tano ndiposa kaunti 11 ndogo zote zipate kadiri ya bilioni sita kila moja. Hilo litaonesha nia nzuri upande wa Kamati. Tunawauliza wasonge tu kidogo ifikie bilioni tano ili kaunti hizo ziridhike. Haya ni kwa sababu hata hizo kaunti zina majukumu mengi Ukitembelea Laikipia, hospitali zetu hazina dawa, barabara hakuna na shida ni nyingi. Kaunti ile ni kubwa sana na majukumu ambayo gavana anapaswa kutekeleza hayatoshelezwi i na hela zilizopendekezwa. Ndiposa kila mtu katika gatuzi anasema kwamba anangoja Rais aje afanye miradi. Wanatutuma kwa Rais ili aende akafanya ilhali gavana yuko pale. Ni kwa sababu hela nyingi zimebaki katika Serikali kuu. Ni jukumu letu kama Seneti kusema kuwa hela zinapaswa kufuata majukumu. Mfano ukulima umegatuliwa. Mambo ya masoko yamegatuliwa lakini majukumu hayo yanatekelezwa na Serikali ya Kitaifa. Hayo ni mambo tunayopaswa kuangalia hapa. Bi. Spika wa Muda, ninapendekeza rekebisho moja. Badala ya shilingi bilioni mbili ya usawazishaji kwa kuinua kaunti zilizo chini ninapendekeza kuongezwe ziwe shilingi bilioni tano na hilo linawezekana. Tusiseme tu hayo. Tueleze kinagaubaga kwa sababu kiwango kilichopendekezwa ni Kshs405 bilioni. Tunapaswa kusukuma zaidi kwa"
        },
        {
            "id": 1570378,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570378/?format=api",
            "text_counter": 269,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "The electronic version of the Senate Hansard Report is for information purposesonly. A certified version of this Report can be obtained from the Director, Hansard and AudioServices, Senate."
        },
        {
            "id": 1570379,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570379/?format=api",
            "text_counter": 270,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Kinyua",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "sababu Seneti ilipitisha kuwa tunataka shilingi billion 465 na hiyo inawezekana tukifanya pamoja. Seneti iliyopita tulitembea pamoja na tukawa na kauli mbiu kuwa hakuna kaunti inayopaswa kupoteza hela. Bi. Spika wa Muda, nataka kuongea na Sen. Mungatana. Tulipofanya hivyo Seneti iliongeza ugavi wa pesa kwa shilingi bilioni 50. Hata sasa tuna uwezo tukitembea pamoja na tukiwa na nia kwa sababu umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Ninawaomba Maseneta wenzangu, tusiseme kuhusu shilingi bilioni nne na tano. Tulenge shilingi bilioni 465 kwa sababu, hili ndilo jukumu letu kubwa katika Seneti hii, kutetea gatuzi. Bi. Spika wa Muda, siku ya leo, Mswada tunaojadili leo ni mwafaka. Huu Mswada ndio umetuleta Seneti hii. Haijali mambo mengine yeyote. Hayo mambo mengine yawe kando kwa sababu, maneno tunayoongea kuhusu makaunti, vile kutafanyika na kutekelezwa, kutatekelezwa kulingana na hela ambazo siku ya leo tunatetea hapa. Hakuna mambo mengine tunapaswa kufanya kwa sababu, leo tunafaa kuongea kuhusu hizi hela na tukipata zile hela tunazozitaka, ziende kule gatuzi. Kuna mambo ya ufisadi na kuvuja kwa hela na hayo yatafwatiliwa na Kamati husika iliyowajibika vilivyo. Lakini, sisi tunafaa kutetea pesa ziende kwa kaunti. Hatuwezi tukasema kuna ufujaji wa hela na ufisadi kwa kaunti zetu, kwa hivyo, hatutatetea pesa. Si gatuzi zote zinafuja pesa. Kuna gatuzi zinafanya kazi vizuri, walio waeredi na stadi kwa kazi waliochaguliwa kufanya. Bi. Spika wa Muda, nitakwamwa hapa nikiwarai Maseneta wenzangu, haswa, Seneta wa Tana River pamoja na Seneta Mandago, wakubali hii jedwali, mahali pa udhibitisho ili tusawazishe kaunti hizi, tupewe bilioni tano. Ndio Seneta Mungatana akitembea Laikipia, apate barabara. Ukitembelea zahanati zetu, upate dawa. Sitaki kumwambia Seneta Mandago kwa sababu, yeye ni mwenzetu n ani jirani pia. Yeye siwezi kumhubiria, tayari ameokoka. Asante, Bi. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii. Pia, ninaunga mkono ikiwa marekebisho ya bilioni tano katika jedwali hii yatafanywa."
        },
        {
            "id": 1570380,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570380/?format=api",
            "text_counter": 271,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Mumma",
            "speaker_title": "The Temporary Speaker",
            "speaker": null,
            "content": " Sen. Mandago."
        },
        {
            "id": 1570381,
            "url": "http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1570381/?format=api",
            "text_counter": 272,
            "type": "speech",
            "speaker_name": "Sen. Mandago",
            "speaker_title": "",
            "speaker": null,
            "content": "Thank you, Madam Temporary Speaker. This is an important Report that has been tabled by the Committee on Finance and Budget, which goes to give resources to our counties. From the onset, I agree with my colleagues who have advanced their argument that the so-called small counties be allocated a minimum of Kshs6 billion. It is not too much to ask. I say that, not because I am against any county from getting any allocation, I say that as a Kenyan who has trans-versed this country and understands the challenge the so-called small counties undergo. I will say the following in support of additional allocation of funds to the small counties. If you look at the cost of development for similar works, like the cost of doing a road in a county like Elgeyo-Marakwet; one kilometre of road to cut through the hills will cost the county government - we are just talking of rural access roads, we are not talking about paved roads - will cost not less than Kshs5 million to do a kilometre of murram road."
        }
    ]
}