{"id":1005385,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1005385/?format=json","text_counter":321,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Asante, Bi Naibu wa Spika, kwa kunipa fursa hii kuchangia Arifa iliyoletwa Bungeni na Sen. Cherargei. Maswala ya rasilimali za nchi na maeneo ambayo zipo ni swala nyeti sana katika nchi yetu. Tumeona kwamba rasilimali nyingi ambazo ziko katika nchi hazifaidi watu wetu ambao wako katika maeneo yale ambayo zinatoka."}