{"id":1011677,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1011677/?format=json","text_counter":294,"type":"speech","speaker_name":"The Temporary Speaker","speaker_title":"","speaker":null,"content":"(Sen. (Dr.) Mwaura): Asante sana Naibu Mwenyekiti kwa Ripoti hiyo ambayo ni nzuri. Ni wazi kwamba Wakenya wengi wanapendelea kuleta mambo yao katika Bunge la Seneti. Ningeomba wale Wenyekiti wanaofuata kufupisha Ripoti zao kwa sababu ya muda. Nampa nafasi Sen. Halake kuwakilisha Kamati ya Mawasiliano na Teknolojia."}