{"id":1014961,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1014961/?format=json","text_counter":479,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Nilibahatika kuandamana na Kamati katika ziara yao ya Kaunti ya Mombasa, Kilifi na Tana River. Tulizuru Mombasa kwa arifa ya siku moja. Tulipozuru Coast General Teaching and Referral Hospital, ambapo vifaa vingi vilikua vimewekwa, Kamati iliridhika na matumizi ya vifaa vile. Vifaa katika hospitali hiyo vilikua vinatumika vilivyo."}