{"id":1018265,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1018265/?format=json","text_counter":118,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr.) Mwaura","speaker_title":"","speaker":{"id":13129,"legal_name":"Isaac Maigua Mwaura","slug":"isaac-mwaura"},"content":"Nakubaliana na Sen. Iman kwamba ni vizuri kuangalia jinsi ambavyo data inatumiwa hususan kwa mambo ya ununuzi katika soko huria zilizoko ulimwenguni. Hata hivyo isiwe kama vita kati ya iPhone na Huawei. Hii ni kwa sababu Uchina inaingiliwa kwa sababu wameanza kuchukua soko ambazo zilikuwa zimedhaminiwa na nchi za kimagharibi. Isiwe ni kisingizio cha kuwaharibia jina kwa sababu nchi kama Marekani ina bejeti maalum ya kupinga utumiaji wa bidhaa kutoka Uchina."}