{"id":1019139,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1019139/?format=json","text_counter":209,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Ndugu yangu ni mwanasheria shupavu na alikuwa katika lile Bunge ambako Gavana Oparanya alikuwa ndani ya Serikali kama waziri. Gavana wangu pia alikuwa Waziri katika hiyo Serikali. Ninamwambia ndugu yangu asifuate sheria hiyo iliyotolewa na Gavana Oparanya kwa sababu haina msingi wa kisheria katika Kenya."}