{"id":1034628,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1034628/?format=json","text_counter":106,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Olago Aluoch","speaker_title":"","speaker":{"id":5,"legal_name":"John Olago Aluoch","slug":"john-aluoch"},"content":"(Kisumu Magharibi, FORD-K); Mhe. Spika, tulipozindua hivi majuzi Kanuni zetu za Kudumu za Bunge la Kitaifa, kumekuwa na tetezi ya kwamba Wabunge wengi kutoka eneo la Nyanza sio wabobea wa lugha ya Kiswahili. Kuthibitisha ya kwamba huo si ukweli kabisa, ningependa kuuliza Swali langu kwa lugha yetu ya kitaifa ya Kiswahili, tafadhali."}