{"id":1037192,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1037192/?format=json","text_counter":560,"type":"speech","speaker_name":"The Temporary Speaker","speaker_title":"","speaker":null,"content":"(Sen.(Dr.) Mwaura): Kwenye orodha yangu hapa, nina Maseneta wanne ambao nitawapa kila mtu dakika tano. Nimekubali kwa sababu pia ya weledi wa lugha na umahiri wako na vile ambavyo una haiba nzuri. Sen. Cherargei, kijana mtanashati, una dakika zako tano."}