{"id":1054576,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1054576/?format=json","text_counter":174,"type":"speech","speaker_name":"Nyali, Independent","speaker_title":"Hon. Mohamed Ali","speaker":{"id":13455,"legal_name":"Mohammed Ali Mohamed","slug":"mohamed-ali-mohamed"},"content":" Mhe. Spika, kauli mbiu ya mimi kuzungumza ni kusema kwamba Bunge hili la 12 limedharauliwa sana kiasi cha kwamba hata sheria zikiundwa humu, hazifuatiliwi wala kutekelezwa. Tunaloliuliza ni kwamba iwapo Mbunge yeyote atauliza maswali yake kuhusiana na eneo lake ama suala lolote linalohusu nchi hii, ni sharti mawaziri waheshimu Bunge hili."}