{"id":1056263,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1056263/?format=json","text_counter":508,"type":"speech","speaker_name":"Hon. (Ms.) Janet Nangabo","speaker_title":"","speaker":{"id":1076,"legal_name":"Janet Nangabo Wanyama","slug":"janet-nangabo-wanyama"},"content":"Watu wanaongea kuhusu Pwani. Sio Pwani peke yake ambapo watu wanatumia mihadarati. Ukija upande wa magharibi katika eneo Bunge la Ikolomani ama Kaunti ya Trans Nzoia, utaona kwamba tumepoteza vijana wetu, kwa sababu wanatoka shule na wanatumia mihadarati. Hawamalizi hata masomo yao."}