{"id":1063104,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1063104/?format=json","text_counter":96,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika, marehemu Sen. Haji aliweza kutekeleza mambo hayo yote matatu. Mtoto wake Sen. Haji Abdulkadir Mohamed wakati kulipokuwa na shambulizi la kigaidi aliweza kuwatetea watu ambao hawajua kabisa. Na hiyo ni ishara kwamba ni mtoto mwema. Kwa hiyo, ninamtakia kila la kheri katika jukumu lake jipya kama Seneta wa Kaunti ya Garissa."}