{"id":1066950,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1066950/?format=json","text_counter":46,"type":"speech","speaker_name":"Mhe. Samia Suluhu Hassan","speaker_title":"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania","speaker":null,"content":"Nami kwa sababu ni mpangaji mpya kwenye hizo nafasi, nimeonelea nije kwa majirani kujitambulisha na nimeanza na jirani wa Kenya ambaye ni jirani ndugu. Nilipata mialiko mingi lakini nilisema eti nianze na hapa. Sijaanza na Kenya kwa sababu ni karibu kijografia, bali ni kwa sababu ya umuhumi na nafasi ya Kenya kwa Tanzania."}