{"id":1068906,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1068906/?format=json","text_counter":124,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika, vifungu ambavyo vinaangazia marekebisho ya Kabtiba vinaanzia 255 hadi 257. Kifungu cha 257 kinazungumzia kurekebisha Katiba kupitia popular initiative. Kifungu cha 257 kinasema kwamba ikiwa moja kati ya Nyumba mbili za Bunge itakataa kupitisha Katiba hii--- Marekebisho yanayoambatana na Kifungu 251(1) ni lazima yafanyiwe kura ya maoni, yaani referendum."}