{"id":1068907,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1068907/?format=json","text_counter":125,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Iwapo tutapitisha ama tutakataa, ni lazima marekebisho haya yaende kwa wananchi kupitia kura ya maoni, kwa sababu ni mambo ambayo tunataka kurekebisha, na yanaingia katika msingi wa Bunge. Sisi kama Bunge tuna jukumu muhimu katika swala hili."}