{"id":1084009,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1084009/?format=json","text_counter":166,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Bi. Spika wa Muda, nilikuwa ninasema kuwa barakoa ambazo sisi tumevaa hazivaliwi kule mashinani. Watu wengine wanavaa hizi barakoa kwa sababu ya kuwaogopa polisi na kuwa wanaendelea na biashara zao. Wakiwaona polisi barabarani wanakumbuka kuvaa barakoa zao. Wanaweza kuokota barakoa yeyote barabarani na kuvaa bila kujali kama imetumika au la."}