{"id":1084183,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1084183/?format=json","text_counter":340,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Wengi wa waathiriwa wa ukimwi wanahudumiwa nyumbani kwao. Wale wanaofanya kazi hiyo ni watu wanaojitolea kufanya kazi bila malipo. Kwa hivyo, Mswada huu utasaidia pakubwa kuwaweka katika hali ya kuridhisha kikazi na vile vile kihuduma kwa wananchi wetu."}