{"id":1087392,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1087392/?format=json","text_counter":169,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Pia ninachukua fursa hii kukemea kauli ya Jaji Mkuu anaposema kwamba Bunge halina nafasi ya kuchunguza Tume ya Mahakama. Tume zote zinapokea ruzuku kutoka kwa Serikali. Tume ya Mahakama ni moja ya tume za kikatiba na zinazotakikana kupeleka tarakimu zake kwa Bunge."}