{"id":1100317,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1100317/?format=json","text_counter":254,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Upande wa Tana River hali ni ngumu zaidi na hali kama ya Laikipia inawakumba wafugaji. Kiangazi ni kikali na malisho ni haba. Hata mahali pa kupata maji hasa upande wa Galana-Kulalu ambapo mradi wa Serikali unafanyika, ng’ombe wanashindwa kuufikia Mto wa Sabaki. Haki haipatikani kwa sababu kuna mradi wa Serikali unaofanyika upande huo."}