{"id":1100321,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1100321/?format=json","text_counter":258,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Hivi majuzi Rais wa Kenya alitangaza hicho kiangazi cha Tana River kama janga la Kitaifa. Kama hali hiyo itakuwa hivyo, basi watu waruhusiwe kuingia katika Mbuga ya Tsavo Mashariki, walishe mifugo kwa sababu kuna nyasi upande huo. Ng’ombe wa watu wanaoishi upande huo hawana lishe. Ninaunga mkono."}