{"id":1109057,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1109057/?format=json","text_counter":20,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Mhe. Spika, maswala ya ajira ni maswala ambayo yako katika kaunti zote katika Jamhuri yetu ya Kenya. Ijumaa iliyopita tulikuwa Mombasa na Kamati ya Seneti ya Ajira, Maswala ya Wafanyikazi na Huduma za Jamii, ambapo tulikuwa tunachunguza maswala ya kudhulumiwa kwa wavuvi ama mabaharia wa Kenya ambao wanafanya kazi katika meli za Wachina."}