{"id":1109323,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1109323/?format=json","text_counter":286,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Sisi hatuna budi kuongeza sauti yetu kwa sababu tunaelewa kuwa walimu ni wengi katika taifa la Kenya. Katika siasa, wengi ndio huhesabika. Tutasimama na walimu usiku na mchana, wakati wanapoenda kusherekea siku yao ya Walimu Ulimwenguni. Hongera walimu wote wa Kenya na duniani."}