{"id":1120113,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1120113/?format=json","text_counter":381,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bwana Spika wa Muda, kuna wale ambao wanataka kuongea kwa muda mrefu. Hatuwakatazi kwa sababu ni haki yao ya kidemokrasia katika Bunge hili. Kuna wale ambao wanataka kuongea kwa muda mchache. Kuweza kupata ule uwiano, wale ambao wanataka kuongea kwa muda mchache wapewe nafasi waongee waondoke. Wale wanataka dakika 10 au 20 watamaliza."}