{"id":1129906,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1129906/?format=json","text_counter":135,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bi. Naibu Spika, nilipendezwa na mwongozo wake katika maswala ya afya ambapo amejenga hospitali kadhaa katika Kaunti ya Jiji la Nairobi. Sehemu nyingi za Nairobi zilikuwa hazina huduma za afya na aliweza kuzifikisha huduma hizo. Vile vile kina mama wajawazito waliojifungua walitajwa. Mhe. Rais alionyesha kuna kazi kubwa ambayo ameifanya lakini bado kuna mengi yanastahili kufanywa."}