{"id":1129914,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1129914/?format=json","text_counter":143,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kwa sasa, hakuna yeyote ambaye amesimamishwa kazi ama kuzuiliwa au kushtakiwa kwa masuala ya ufisadi. Ufisadi ni donda sugu ambalo lazima Serikali hii na Serikali zitazokuja liweze kudhibiti. Bila kufanya hivyo, Wakenya wengine wataendelea kulia bila ya kupata huduma wanazostahili kupata kwa sababu ya ufisadi."}