{"id":1135680,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1135680/?format=json","text_counter":219,"type":"speech","speaker_name":"Sen Wetangula","speaker_title":"","speaker":{"id":210,"legal_name":"Moses Masika Wetangula","slug":"moses-wetangula"},"content":"Bw. Spika, tukielelekea katika uchaguzi mkuu, tunakuunga mkono vile umekuwa ukisema mara kwa mara ya kwamba tunahitaji uchaguzi wenye usawa, haki, ukweli na amani. Hii ni kwa sababu nchi yetu imepitia changamoto kubwa ya mabishano ya uchaguzi mwaka wa 2007 mpaka tukapoteza maisha na mali ya Wakenya."}