{"id":1135687,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1135687/?format=json","text_counter":226,"type":"speech","speaker_name":"Sen Wetangula","speaker_title":"","speaker":{"id":210,"legal_name":"Moses Masika Wetangula","slug":"moses-wetangula"},"content":"Alliance (OKA); ndugu zangu, Mhe. Kalonzo Musyoka, Mhe. Musalia Mudavadi, Sen. Gideon Moi, Mhe. Cyrus Jirongo na wale wote ambao wamesema wataungana na sisi. Tunawaomba tuchangie vilivyo kama Wakenya wengine tukijua uchaguzi unakuja na lazima uwe wa haki, usawa, ukweli na wa amani. Bw. Spika, Mungu atubariki sisi sote. Turudi mwezi ujao kama Maseneta tukijua ya kwamba leo tumepigania kuongeza pesa kwa kaunti zetu. Tuwe na huo msimamo, kwa sababu kama uchumi umekuwa, lazima kaunti pia zipate mapato yanayokua. Asante, Bw. Spika."}