{"id":114766,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/114766/?format=json","text_counter":260,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"(Mr. A.C. Mohamed):Asante sana, Bw. Naibu Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii niungane na wenzangu ili niweze kumpongeza Rais kwa Hotuba yake ya kusisimua aliyoisoma hivi majuzi. Hotuba yake imegusia mipangilio ya maendeleo katika sehemu zote za Kenya. Ametuhimiza tuwe na umoja wa dhati katika kujenga taifa hili, na vile vile tusitumie siasa ili kuweza kuwagandamiza wanasiasa wengine kwa sababu hii au nyingine."}