{"id":1163074,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1163074/?format=json","text_counter":88,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bi. Spika wa Muda, wiki tatu nyuma, swala hili lilipozungumziwa, tulipitisha kwamba Spika awasiliane na Wizara husika na kwamba sisi kama Maseneta tunaweza kuchukua ruhusa kwa Spika pekee yake. Hatuna jukumu la kuchukua ruhusa kwa taasisi nyingine yeyote."}