{"id":1163099,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1163099/?format=json","text_counter":113,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Boy","speaker_title":"","speaker":{"id":13200,"legal_name":"Issa Juma Boy","slug":"issa-juma-boy"},"content":"Alipokuja nikashangaa na kujiuliza kulikuwa na shida gani. Aliniambia niende kwa ofisi. Nikaingia kwa ofisi yake na akaniambia ya kwamba anasikitika kwamba sitoweza kuruhusiwa kwenda safari yangu kwa sababu wamepata mwelekeo kwamba Maseneta hawawezi kuruhusiwa kusafiri kwa ule mda."}