{"id":1163536,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1163536/?format=json","text_counter":49,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Asante, Bi. Naibu Spika. Kwanza, nataka kutoa kongole kwa walimu ambao walijitoa mhanga kufundisha watoto wadogo katika shule za chekechea. Tunaelewa hiki ni chama cha walimu wa shule za chekechea na ni wanachama wa kile chama cha walimu."}