{"id":1163749,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1163749/?format=json","text_counter":262,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wario","speaker_title":"","speaker":{"id":13224,"legal_name":"Golich Juma Wario","slug":"golich-juma-wario"},"content":"Sijui kama hilo linawezekana hapa Afrika kwa sababu ukipeleka wazee mahali moja, wanaweza kukataa wakidhani kuwa wanaenda kutupwa kama takataka. Tukipendekeza kuwa na makao ya wazee, vijana wengine ni vichwa maji. Wanaweza kubeba wazee kwa lori na kuwapeleka huko. Pengine hiyo inafaa kuwa tu kwa Wazungu kwa sababu haitufai sisi."}