{"id":1169314,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1169314/?format=json","text_counter":305,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kama tunavyojua, seli za polisi hazina vyumba tofauti vya wafungwa. Wafungwa wote wanawekwa pamoja kama mahabusu na labda yule mtoto hakufanya uhalifu wowote. Lakini, atakapotoka pale, kwa sababu ameingiliana na wahalifu, anaanza kuwa na hulka za kuwa mhalifu."}