{"id":1169643,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1169643/?format=json","text_counter":272,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bi. Spika wa Muda, haya maswala mengine ni ya uchumi wa ulimwengu. Kwa mfano, tatizo la ongezeko la bei za chakula. Hili tatizo haliadhiri Kenya peke yake. Linaadhiri nchi zote ulimwenguni. Tatizo la ongezeko la bei ya mafuta haliadhiri Kenya peke yake. Linaadhiri nchi zote hususan zile nchi ambazo zinandelea."}