{"id":1170289,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1170289/?format=json","text_counter":95,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Bw. Spika, asante kwa kunipa fursa hii. Kwanza kabisa ninatoa risala zangu za rambirambi kwa jamaa na familia waliopoteza wapendwa wao. Ni jambo la kuhuzunisha sana. Jambo ambalo linaudhi ni kwamba wale watu kutoka Masimba, walikua wakiandamana kisheria. Sheria zetu zinaruhusu mtu yeyote kufanya maandamano. Kisa na maana ya wao kuandamana ni wenzao saba kuvamiwa na kuuawa na ndovu."}