{"id":1176627,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1176627/?format=json","text_counter":458,"type":"speech","speaker_name":"Sen. (Dr) Khalwale","speaker_title":"","speaker":{"id":170,"legal_name":"Bonny Khalwale","slug":"bonny-khalwale"},"content":"Bw. Spika wa Muda, namshukuru ndugu yangu Justice Madzayo kwa msimamo wake. Sina shaka naye. Lakini ningependa kumkumbusha kwamba wale ambao walimtangulia kama sisi, tumekuwa huko, tukajaribu. Kuwa huko upinzani ni sawa na kuoa mwanamke mwanamwali ambaye ni tasa. Ninamwomba Seneta wa Baringo kuafiki Hoja hii."}