{"id":1179925,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1179925/?format=json","text_counter":331,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Miraj","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Asante, Bw. Spika wa Muda, kwa kunipa fursa hii niweze kuchangia Hoja hii. Naunga mkono Hoja hii ya Seneta mwenzetu. Ni kinaya kwamba miaka 60 baada ya Kenya kujikwamua kutoka kwenye minyororo ya mabepari, tunazungumza juu ya masuala ya ukame na ukosefu wa lishe ya kutosha katika taifa letu."}