{"id":1181050,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1181050/?format=json","text_counter":90,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Mswahili anasema kuwa “mtoto akikosa maziwa ya mama, hata ya mbwa ni maziwa.” Kwa hivyo, ni vizuri, hata ijapokuwa tunaunga mkono kwa sababu ya mazingira haya mazuri, lakini mazingira yakiwa hata mazuri namna gani na mtu ana njaa haitakuwa na faida yeyote kwake."}