{"id":1185816,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1185816/?format=json","text_counter":61,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Mgogoro huu wa shamba la Ruaraka ulichunguzwa na Kamati iliyoongozwa na Seneta wa Homa Bay, Sen. M. Kajwang’. Baadhi ya mapendekezo kwenye Ripoti ya Kamati ilikuwa wale wote walihusika katika malipo ya ile ardhi ya Ruaraka wachunguzwe na wafunguliwe mashtaka kutokana na ulipaji wa pesa taslimu billioni moja na laki tano za Kenya kwa ardhi ya serikali."}