{"id":1192069,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1192069/?format=json","text_counter":86,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Mwisho, Bw. Spika, ni kwamba wakati watoto hao wanapokua, ni vigumu sana kupata vyeti kuonyesha kwamba ni walemavu. Lazima mtoto kama huyo alipe Kshs1,500 katika hospitali za kaunti ili apewe cheti cha kuonyesha kwamba ni mlemavu, ndiposa aweze kupata marupurupu ama fadhila zingine za kuonyesha kwamba ni mlemavu. Katika jamii, sisi tunatakikana tuwasaidie zaidi kuliko tunavyojisaidia sisi wenyewe. Bw. Spika, naunga mkono Taarifa hii."}