{"id":1196772,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1196772/?format=json","text_counter":148,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Harambee Stars. Kwa bahati mbaya, umri ukawa haumruhusu. Hivyo basi, hakuweza kuingia katika Harambee Stars. Sen. Murkomen ni mtu ambaye anachukulia watu wote kwa usawa na ana heshima kwa binadamu. Kwa hivyo, twamtakia kila la heri katika nyadhifa yake mpya ya Uwaziri. Bw. Naibu Spika, Serikali iliyoondoka imefanya miradi mingi katika Kaunti ya Mombasa. Na sisi tunataka ile imebakia, Sen. Murkomen, ambaye ni Waziri wa Barabara aimalize, ili Mombasa iweze kuwa shwari kama hapo awali."}