{"id":1197680,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1197680/?format=json","text_counter":222,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kuvunjiliwa mbali kwa kitengo hicho hakutatatua maswala haya. Hii ni kwa sababu, Serikali ambayo ilikuwa mamlakani ilikuwa ni “nusu mkate” kuanzia mwaka wa 2013 mpaka 2022. Kwa hivyo, walihusika kwa kiwango fulani kwa vitendo hivi vya maafisa wa usalama."}