{"id":1209411,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1209411/?format=json","text_counter":246,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Pili, ningependa kumwambia Gavana Kawira ambaye yuko hapa mbele yetu na pia bunge la kaunti kuwa sio kwamba mmoja ameshinda na mwengine ameshindwa. Mumeletwa pamoja na kuzinduliwa kwamba mmechaguliwa kutumikia wananchi wa Meru na wa Kenya kwa jumla. Kwa hivyo, hapa hakuna mshindi. Walioshindwa ni wakaazi wa Meru amabao wamekosa huduma kwa muda wa miezi minne sasa."}