{"id":1209747,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1209747/?format=json","text_counter":217,"type":"speech","speaker_name":"Hon. Kingi","speaker_title":"The Speaker","speaker":null,"content":"kusema ati hata hilo jopo liongezewe nafasi kwa sababu wewe, Bw. Spika, ni mwanasheria, Wakenya wataona kwamba unapendelea wengine. Bw. Spika, ninataka tu kuwa upande wako ndio usije ukaonekana kana kwamba unapendelea wengine. Sisi hatuna shida na wanasheria kwa sababu hao ndio huwa wanatutea wakati tuko na shida. Hata hivyo, wazingatie Wakenya wengine ambao sio wanasheria."}