{"id":1210068,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1210068/?format=json","text_counter":260,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Bw. Mwenyekiti wa Muda, lile linalotusumbua si vile picha ilivyokua, ila ni ile lugha Seneta wa Nairobi alitumia. Aliita Mwenyekiti anayeongoza Bunge hili mwongo. Haikubaliki! Tutakubali kwanza ikiwa Seneta wa Nairobi akiomba msamaha kwa kutumia lugha isiyokubalika katika Bunge hili. Baadaye, zile picha zinaweza kuletwa. Aliyesema hizo picha si nzuri ni Kiongozi wa Walio Wengi na amevaa miwani. Kwa hivyo, anaweza kosa kuona vizuri."}